Monday 3 September 2018

JESHI LA MAGEREZA LAVUTIWA NA TEKNOLOJIA YA UJENZI WA GHARAMA NAFUU

Jeshi la Magereza (Tanzania Prison Service) haliko nyuma katika kusambaza teknolojia ya ujenzi wa nyumba bora na za gharama nafuu. Baadhi ya Askari wa Jeshi hilo kutoka Lindi na Tanga walifika NHBRA kuanzia tarehe 20/08/2018-02/09/2018 kwa ajili ya kupata mafunzo ya namna ya kutumia mashine ya matofali ya kufungamana na jinsi ya kujenga kwa kutumia tofali hizo ambapo pia waliahidi kusambaza teknolojia hii kwa jamii iliyowazunguka. 

Askari kutoka Jeshi la Magereza wakiwa kwenye jaribio la kufyatua tofali la kufungamana katika ofisi za NHBRA






Washiriki kutoka Jeshi la Magereza wakitoa tofali la kufungamana kutoka kwenye mashine ya matofali ya kufungamana

Askari wa Jeshi la Magereza wakifanya setting ya nyumba katika mafunzo ya ujenzi wa nyumba kwa kutumia matofali ya kufungamana yanayotolewa na NHBRA







Ili kuweza kupata mafunzo kama haya, mteja unashauriwa kununua mashine ya matofali ya kufungamana kwa gharama ya shilingi 650,000/- ambapo malipo hayo mteja atapaswa kulipia benki. Na baada ya kununua mashine Mteja atapata mafunzo kwa vitendo juu ya utumiaji wa mashine ya tofali za kufungamana pamoja na namna ya kujenga kwa muda wa wiki moja kulingana na uelewa wa vijana ambao Mteja atakuwa amewaleta wasiozidi watatu.

Kwa mawasiliano zaidi, usisite kututafuta kwa namba ifuatayo;

0679972715

au

Barua pepe: dawatilamsaada@nhbra.go.tz

au

Fika ofisini kwetu Mwenge tunapakana na kituo cha mafuta cha Oilcom.

Karibuni sana.

No comments:

Post a Comment