Tuesday 17 April 2018

USAMBAZAJI WA TEKNOLOJIA YA UJENZI WA GHARAMA NAFUU

Moja wapo ya jukumu la Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi ni kusambaza matokeo ya tafiti zake kwa njia mbalimbali ikiwemo kutoa mafunzo kwa vikundi au mtu mmoja mmoja.

Pichani ni baadhi ya vikundi vilivyotutembelea katika ofisi zetu Mwenge, Dar es Salaam kwa ajili ya kupata mafunzo juu ya ujenzi wa gharama nafuu kwa kutumia matofali ya kufungamana pamoja na vigae mkonge.




Kwa mawasiliano zaidi juu ya namna ya kupata mafunzo na kununua mashine za matofali ya kufungamana au vigae mkonge, usisite kututafuta;

Barua pepe: dawatilamsaada@nhbra.go.tz

Namba ya Simu: +255 679 972 715