Tuesday 18 September 2018

KAIMU MKURUGENZI WA NHBRA ATEMBELEA KARAKANA NA WAKALA

Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi (NHBRA) Bw. Dismass Minja, alipata nafasi ya kuangalia baadhi ya Tafiti zilizofanywa na Wakala pamoja na Tafiti nyingine zinazoendelea.

Meneja wa Utafiti Eng. Benedict Chilla akitoa maelezo ya Tafiti zinazoendelea juu vigae vya kuchoma, kwa Kaimu Mkurugenzi wa Wakala Bw. Dismass Minja 


Kaimu Mkurugenzi wa NHBRA akiangalia utengenezaji wa ''Waffles'' ambayo pia ni miongoni mwa Tafiti zilizokamilika. Teknolojia hii mpya kwa Tanzania hutumika zaidi katika ujengaji wa nyumba za ghorofa 

Fundi Sanifu akitoa maelezo juu ya mashine ya kufyatulia matofali ya kufungamana ambayo bado iko kwenye tafiti yenye uwezo wa kutoa matofali mawili.

Meneja Utafiti na Maendeleo akitoa maelezo kwa Kaimu Mkurugenzi juu ya utengenezaji wa kigae mkonge




Kaimu Mkurugenzi akiangalia fremu ya mlango wa zege ambayo tayari imeshawekwa ukutani. Fremu hizo zimeonekana kuwa zitakuwa suluhisho kubwa kwa Watanzania wanaolalamika mchwa kuharibu milango yao
Kaimu Mkurugenzi akiangalia ufyatuaji wa tofali la kufungamana


Kaimu Mkurugenzi akifanya jaribio la kutoa tofali katika mashine ya kufungamana

Kwa mawasiliano zaidi juu ya namna ya kupata mashine ya matofali ya kufungamana, kununua tofali, vigae mkonge na kupata mafunzo usisite kututafuta kwa namba ifuatayo;

0679972715

au

Barua pepe: dawatilamsaada@nhbra.go.tz

au

Fika ofisini kwetu Mwenge tunapakana na kituo cha mafuta cha Oilcom.

Karibuni sana.

No comments:

Post a Comment