Thursday 5 May 2016

UJENZI WA NYUMBA KWA KUTUMIA MATOFALI YA KUFUNGAMANA (INTERLOCKING BRICKS)


Ujenzi wa nyumba kwa kutumia matofali ya kufungamana ni mojawapo ya aina ya ujenzi wa gharama nafuu ambao huondoa matumizi ya udongo mwashi kama kiunganishi kati ya tofali na tofali ingawa mambo yote ya msingi na kanuni za ujenzi lazima vizingatiwe.
Kabla ya kuanza ujenzi ni lazima kuwe na msingi imara uliojengwa kwa vifaa imara ambao upo kwenye vipimo sahihi, ili kuweza kutumia tofali hizi. Sehemu ya msingi wa nyumba (substructure) itakuwa na-:

      Kitako cha msingi: zege/mawe
      Ukuta wa msingi: Matofali ya saruji na mchanga, udongo na saruji yanayofungamana, mawe au matofali ya kuchoma.
 
Endapo tofali za udongo-saruji za kufungamana zitatumika ni lazima unene wa ukuta wa msingi usipungue sm 30 (urefu wa tofali). Ili kukabiliana na hali ya unyevunyevu ni vyema kuimarisha zaidi tofali kwa kuongeza kiwango cha saruji kwenye udongo wakati wa ufyatuaji.
Ujenzi kwa kutumia matofali ya udongo au udongo ulioimarishwa umeonekana kuwa wa gharama nafuu zaidi kutokana na upatikanaji wa udongo katika sehemu kubwa nchini.
 
Katika ujenzi huu tofali linalotumika huwa na vipimo vifuatvyo:

      Urefu 300mm
      Upana 150mm
      Unene 100mm

Vilevile kuna vipande vya nusu na robo tatu tofali.
 
Tofali Zima
 

Robotatu tofali
 
Nusu tofali
 
Tofali Zima
 
Robotatu tofali mbili

Tofali la chaneli
 
Kabla ya kuanza ujenzi ni lazima kupitia ramani iliyopo ili kuona kama inakubaliana na vipimo vya urefu wa ukuta ambapo ni lazima vigawanyike kwa  tofali zima au nusu (yaani 300 au 150mm).

Mfano ukuta wenye urefu wa mita 3, hujengwa kwa tofali nzima 10, katika mstari mmoja wenye urefu huo. Ikumbukwe kuwa katika ujenzi huu hatukati vipande vyenye urefu mbalimbali kama ambavyo hufanyika katika ujenzi wa matofali yasiyofungamana, badala yake vipande vya nusu na robo tatu hutumika.
Nyumba imegawanyika katika sehemu kuu mbili:-

      Msingi:        Sehemu ya chini ya nyumba (substructure)
      Boma:         sehemu ya juu ya msingi
Msingi:       Msingi wa nyumba hujengwa kwa:

      zege,
      mawe
      matofali ya saruji na mchanga
      matofali ya udongo na saruji.

Namna ya kuset matofali ya kufungamana kwenye msingi uliojengwa kwa matofali ya saruji na mchanga.

Kwa kuwa msingi ndio sehemu inayobeba mzigo wa jengo zima ni muhimu vifaa vinavyotumika kuujenga viwe bora na imara. Kwa maeneo yaliyo mengi nchini zege, mawe na tofali za saruji mchanga ndio hutumika kujenga msingi wa nyumba. Hata hivyo matumizi ya udongo na saruji hutumika kujenga misingi kwa maeneo yenye udongo imara. Lakini mchanganyiko wake ni lazima uboreshwe zaidi ili kupata tofali imara lenye uwezo wa kubeba uzito na kuhimili hali ya unyevunyevu.

Boma: Sehemu hii ya nyumba hujengwa kwa kutumia zege, mawe, matofali ya mchanga na saruji, matofali ya udongo na saruji, matofali ya udongo na chokaa au matofali ya udongo. Ujenzi kwa kutumia matofali ya udongo au udongo ulioimarishwa umeonekana kuwa wa gharama nafuu zaidi ukilingnisha na ujenzi wa matofali ya saruji na mchanga. (itaendelea toleo lijalo)

Boma lililojengwa kwa kutumia matofali ya kufungmana
Usikose mwendelezo wa mfunzo haya, tukutane toleo lijalo.......

No comments:

Post a Comment